Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Queen Sendige amewataka Wakutubi nchini kuwa kisima cha maarifa kipindi chote wanapokuwa  wanatoa huduma ya kutoa  taarifa kwa wasomaji.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Queen Sendige amewataka Wakutubi nchini kuwa kisima cha maarifa kipindi chote wanapokuwa  wanatoa huduma ya kutoa  taarifa kwa wasomaji.

Mhe. Sendige ameyasema hayo katika hotuba yake ya ufunguzi wa  Mkutano Mkuu wa Chama Cha Wakutubi Tanzani- Tanzania Library  And Information Association (TLA)unaofanyika kwa siku 6 kuanzia  26 Februari - hadi  01 Machi 2024  katika ukumbu wa  KISORA ROYOL HALL Wilayani Babati.

Katika hotuba yake ya Ufunguzi wa Mkutano huo akiwa kama mgeni rasmi Mhe. Sendige  amewashukuru Viongozi wa  Chama Cha Wakutubi Tanzani  (TLA) kwa uamzi wao wa kuchagua Mkoa wa Manyara kuwa Mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Wakutubi Tanzania kwa mwaka 2024.

Aidha Mhe. Sendige amewaasa  Wakutubi kuwa kisima Cha maarifa mengi  kwa kuwa wanahudumia wasomaji mbalimbali wenye uelewa tofauti, hivyo kuwaomba kuwa na maarifa mengi yatakayosaidia kujua vyanzo vingi vya taarifa  ambazo wasomaji wanazihataji kupita kwao.

Aidha  ametoa wito wa  kuanzishwa Maktaba katika Mkoa wa Manyara Ili kuleta chachu ya usomaji katika jamii ya watu wa Manyara zikiwemo taasisi Serikali na  Sekta binafsi.

"Naomba kuwashukuru sana kwa uwepo wenu kwa siku 6 katika Mkoa huu ni heshima ya pekee mmeupa Mkoa wetu heshima ya  kufanya Mkutano wenu ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha usomaji kwa kuwa  maarifa mengi yanapatikana kupitia kusoma vitabu na kupitia vyanzo mbalimbali kulingana na teknolojia tuliyonayo leo" ,Amesema Sendige.

Vile vile Mhe. Sendiga ametoa wito kwa viongozi wa TLA Mkutano ujao uwe na  ushirikishwaji wa wadau wa sekta  mbalimbali  katika Ukutubi ili  wasaidie kutoa maoni yao na kuanisha mapungufu yalipo kusoma vitabu wenyewe kwanza Ili  waweze  kuelewa maarifa yalimo

"Mtakuwa mmefanya jambo la maana sana kama mtawashirikisha wadau wenu wao ndio wanajua mafanikio na mapungufu yenu kuwashirikisha katika vikao vyenu watawasaidia sana kuinua tasania yenu hasa katika kipindi hiki ambacho teknolojia imepiga hautua kubwa" ,Amesema Sendiga

Awali akimkaribisha Mgeni rasmi katika hotuba yake  Makamu mwenyekiti wa TLA  Dkt. Leontine kwa niaba ya Mwenyekiti  wa TLA Prof  Ally Mcharazo ameshukuru Mhe. Sendiga kwa kukubali mwaliko wa kuwa mgeni  rasmi  katika ufungunzi wa Mkutano huo.

Dkt. Leontine ameeleza  kuwa Chama Cha Wakutubi Tanzani (TLA) kilianzishwa mnamo mwaka 1974 kikiwa na Malengo mengi kubwa ikiwa ni kuwakutanisha Wakutubi wote nchini ili waweze kijadili kwa pamoja mikakati na changamoto mbalimbali zinazoikabili Tasnia ya Ukutubi nchini.

Dkt. Nkebukwa ameeleza kuwa Chama Cha Wakutubi Tanzania (TLA) kimekuwa na mwendelezo wa  kufanya mikutano yake kila mwaka kwa kuzunguka Kila Mkoa yote nchini  isipokuwa Mkoa wa Manyara pekee ambao Mkutano huo unafanyika kwa mara ya kwanza.

       MWISHO